Dc Kalambo Awaonya Wazazi na Walezi Wanao Washawishi Wanafunzi Kufanya Mitihani Vibaya


 Na Baraka Lusajo. Kalambo 

Zikiwa zimesalia siku chache wanafunzi wa darasa la saba kuanza mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi,Mkuu wa wilaya ya kalambo Julieth Binyura amewaagiza maafisa elimu wilayani humo kuwachukulia hatua kali za kisheria ikiwemo kuwafikisha mahakamani wazazi na walezi ambao watagundulika kuwashawishi watoto wao kufanya mitihani yao vibaya  kwa lengo la kuwasaidia kazi za nyumbani.

Julieth Binyura-mkuu  wa wilaya ya Kalambo akiongea na  wananchi katika mji wa Matai.
Kumekuwepo na changamoto ya baadhi ya wazazi na walezi wilayani humo kuwashawishi watoto wao kufanya vibaya mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi  kwa lengo la kuwasaidia kufanya kazi za nyumbani zikiwemo kilimo,kuchunga ng’ombe na watoto wa kike  kuwaozesha.

Hali hiyo imepelekea mkuu wa wilaya  hiyo Julith Binyura Kuingilia  kati  swala hilo kwa kuitisha mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata  ya Matai  na  kuwataka wananchi kutoa  taarifa za uwepo  wa  vitendo  hivyo ili wahusika  waweze  kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Amesema  serikali  haita  wafumbia  macho wazazi  na walezi watakaokamatwa   kwa tuhuma za  kuwaachisha  masomo  watoto  wao  kwa  kuwapeleka  mashambani  au  machungani.

‘’kunatabia za baadhi ya wazazi ambao wana waambia watoto mkaandike vibaya vibaya sasa tutakaye mgundua ataenda jela akatumikie kifungo. Hivyo nimarufuku wazazi kuwaambia watoto mkaandike vibaya.
Efraim Moses kaimu mkurugenzi -kalambo
 ‘’Niwatake wanafunzi kutoa taarifa kwa walimu kama wazazi wenu watawashawishi kufanya  mitihani vibaya. Niwatake pia wazazi muwaache wanafunzi wasome kwa amani na tuna imani  mwaka  huu  wanafunzi wote watafaulu’’.alisema Binyura.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Efraim Moses Mwalemba, amesema lengo la  serikali ni kuhakikisha kila mtoto anapata elimu sitahiki.

Amesema  wazazi  wanatakiwa  kuwa   na uelewa  sahihi  juu ya  umuhimu  wa  elimu  kwa  kuwapeleka  watoto wao shule kama Serikali ya awamu ya tano inavyotoa  sera ya  elimu bure kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari

Hata hivyo kwa mwaka 2019 wanafunzi 3724 wilayani humo wanategemea kuanza mitihani yao ya kuhitimu elimu ya  msingi na huku mitihani hiyo ikitegemewa kuanza kufanyika Sptember 11 hadi 12 ,2019.



Comments