Dc Binyura Atoa Siku Saba Kwa Wafanyakazi Wa Kampuni Ya Kichina Kupewa Mikataba.

katika picha ni wafanyakazi wa kampuni  ya  kichina 


 Na Baraka  Lusajo.Kalambo.

Mkuu wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Julieth Binyura ametoa siku saba kwa kampuni ya kichina inayotengeneza barabara ya lami kutoka Sumbawanga-Matai-Kasanga mwambao wa ziwaTanganyika kulipa mishahara pamoja na kutoa mikataba kwa wafanyakazi wao na kuahidi kuwaweka ndani viongozi  wote wa kampuni hiyo endapo watashindwa kutekeleza agizo hilo.
katika picha ni mkuu  waa  wilaya  ya Kalambo Julieth  Binyura.

Kumekwepo na malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wafanyakazi wa kampuni ya kichina ya‘’
Joint Venture of China Railway 15G and new centry co ltd’’ kutotoa mikataba pamoja kutopeleka fedha kwenye mfuko hifadhi wa taifa wa jamii NSSF licha ya wafanyakazi hao kukatwa fedha na kamapuni hiyo kupitia mishara yao na kumtaka  mkuu wa wilaya hiyo kuingilia kati swala hilo.

Awali wakiongea mbele ya mkutano wa hadhara ulifanyika katika kata Kasanga wilayani humo ,wamesema wanahofu na mashaka juu ya kutolipwa sitahiki zao kutokana na mradi huo kutakiwa kukamamilika November 2019 na kuwa kila wakienda NSSF kufuatilia mafao yao wamekuwa wakiambiwa kuwa hakuna fedha zilizoingizwa  kwenye acont zao na mwajiri wao.

Wamesema serikali kupitia mkuu wa wilaya haina budi kuingilia kati swala hilo kwa kutoa maagizo kwa wahusika ili waweze kuingiziwa fedha zao kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii.

Jacksoni Mayunga mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo,amesema licha ya hilo wafanyakazi  waliowengi kwenye kampuni hiyo hawana mikataba na wengine wamekuwa wakifukuzwa kazi bila  kupewa  barua hali ambayo imekuwa ikiwapatia ugumu hususani wakati wa kudai mafao yao NSSF.

Meneja wa NSSF mkoani Rukwa Salawa Hangumbalo,amesema endapo fedha zikipelekwa NSSF  wafanyakazi  wote watalipwa na kuwasihi wafanyakazi hao kufika  kwenye ofisi za mfuko huo kutoa taarifa pindi kunapotokea changamotoa yoyote.
katika picha ni meneja  wa NSSF mkoani Rukwa

mkuu wa wilaya hiyo Julieth Binyura amelazimika Kuingilia kati swala hilo na kutoa siku saba kwa kamampuni hiyo kupeleka fedha kwenye mfuko wa hifadhi  ya jamii wa taifa NSSF pamoja na kutoa barua  za wafanyakazi wote ambao walikuwa  wameachishwa kazi kwa  lengo la kuondokana na migogoro  isiokuwa  ya  lazima.

‘’natoa maagizo  kwa  uongozi  wa  kampuni hii ,nataka ndani  ya siku  saba mtoe barua  kwa  wafanyakazi  wote ambao  walikuwa  wameachishwa  kazi pia mtoa mikataba kwa  kila mafanya kazi wenu na endapo mkishindwa kufanya hivyo mkurugezi wa kamapuni pamoja na viongozi wengine nitawaweka nadani’’Alisema Binyura.

Mradi wa ujenzi  wa barabara ya  lami ya Sumbawanga – Matai – Kasanga yenye urefu wa km107 unafadhiliwa na Serikali ya Tanzania na kugharimu Shilingi Bilioni 133.2 ambapo ujenzi wake unategemewa kumalizika mwezi  November  2019 chini ya Mkandarasi Joint Venture of China Railway 15G/New Century Company Ltd.
0762432747. maswaliano zaidi.

Comments