Chama Cha Mapinduzi CCM Wilayani Kalambo Chajidhatiti Kushinda Kwa Asilimia 99 Katika Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa.



Na Baraka Lusajo. Kalambo.

Chama cha Mapinduzi  CCM Wilayani  Kalambo Mkoani Rukwa kimeuhakikishia umma  kuwa kitashinda  kwa  kishindo  katika uchaguzi wa  serikali za mitaa kutokana na utekelezaji sahihi wa ilani yake ya uchaguzi huku kikiwataka wananchi  kujitokeza  kwa  wingi katika  zoezi la kujiandikisha na kupiga kura  ifikapo 24 Novemba kuwachagua viongozi bora kwa maendeleo ya  Taifa.   
Wilaya ya Kalambo yenyeVitongoji 422, Vijiji 111, kata 23 na Tarafa 4 ambazo ni Kasanga, Matai, Mwimbi na Mambwe, inakadiriwa kuwa na jumla ya watu 271,393 wakiwemo wanaume 131,285 na wanawake 140,108 ambao wote wanatakiwa kuhamasishwa vilivyo ili washiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka huu.

Katibu wa Siasa na Uenezi  Wilayani  Kalambo  John Mbita amesema chama kimejidhatiti vilivyo kuelekea kwenye ushindi kwani Mwenyekiti wa chama hicho kitaifa Mh. Rais Wa Jamhuri ya mungano wa Tanzania Dr,John  Pombe  Magufuli  ametekeleza  kwa  asilimia  mia moja ahadi zote.

 ‘’Kila mwananchi  ana haki sawa ya kugombea na kupiga kura, kama mwana Falisafa mkongwe wa Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Havard Profesa John Luke kupitia nadharia yake ya uwakilishi [Represantation theory]. Hivyo wananchi wote tujitokezeni  kwa wingi katika  kujiandikisha na kupiga kura kwani ni  haki yetu ya msingi ifikapo  tarehe 24 Novemba 2019 ili tupate viongozi bora watakao tuletea maendeleo.’’Alisema mbita.

Wakiongea kupitia maadhimisho ya uzinduzi wa ligi ya mapinduzi Cup yaliyofanyika  katika kata  ya Mwazye Wilayani  humo,viongozi  na makada  wa chama cha mapinduzi  CCM, wamesema kimsingi kila  mwananchi anahaki ya kugombea na kupiga kura.

Comments