Zaidi Ya Kaya 4545 Za Nuafaka Na Mpango Wa Tasafu ‘’Kalambo

kushoto ni mkuu  wa  wilaya  ya kalambo akiongea  na wanufaika  wa tasafu

Na Baraka Lusajo. Kalambo

Mkuu wa wilaya ya kalambo mkoani Rukwa Julieth Binyura amezitaka kaya masikini zinazowezeshwa kupitia mfuko wa tasafu kuzitumia vizuri fedha wanazopatiwa na serikali kwa kuzielekeza zaidi katika shughuri mbalimbali za maendeleo yao binafusi na kuwasaidia kujikwamua na hali ya kiuchumi.

Binyura ameyasema hayo wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayofanywa  wananufaika wa mpango wa tasafu katika vijiji vya Jengeni na Safu vilivyopo mpakani mwa nchi ya Tanzania na Zambia wilayani kalambo mkoani hapa.

Amesema amelazimika kuanzisha oparesheni ya ukaguzi wa wanufaika wa mradi huo kutokana na   kuwepo kwa malalamiko kwa badhi ya maeneo kupewa fedha watu ambao sio walengwa  wa mradi huo.

Mratibu  wa  mradi  tasafu wilayani humo Michael Mwasumbi amesema fedha  hizo hutolewa  kulingana na hali
‘’kwa mwaka 2019 kaya 4545 katika vijiji 66 vimeingizwa kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini , ambapo kiasi  cha  shilingi milioni 1,244,000/=zimelipwa  katika  kijiji cha Jengeni  na kiasi cha  shilingi milioni 1,920,000/= zimelipwa  katika kijiji cha Safu vyote vinapatikana mpakani  mwa nchi  ya Tanzania  na Zambia.’’alisema Mwasumbi.

katikati ni mratibu  wa tasafu  wilayani kalambo akiongea  na wanufaika  wa mpango  wa tasafu
Baadhi ya wanufaika wa mfuko huo wilayani humo wamempongeza Raisi wa jamhuri ya mungano wa Tanzania John Pombe Magufuli kwa kuwapatia fedha hizo kwani zimewasaidia  kwa kiasi  kikubwa katika  kuendeleza  maisha  yao.

katika picha  ni wanufaika  wa mpango  wa tasafu wilayani kalambo
Palizoni Mpinya mnufaika wa  mpango  wa  tasafu  katika  kijiji  cha Jengeni  amesema wanampongeza  Raisi Magufuli kwa  kutoa  fedha  hizo  kwani zimekuwa msaada  mkubwa  katika  maisha yao  kwa ujumla hususani  katika  kusimesha   watoto  waao pamoja  na kuendeleza miradi mingine.

‘’tunasomesha  watoto pia  tunavaa kutokana na miradi ya tasafu, hivyo hatunasababu  ya  kumshukuru mh.Raisi  kwa kutangalia  sisi  wanyonge hususani  katika  kutupatia fedha  hizi.’’alisema mnufaika  huyo.

Comments