Watumishi Walio Masomoni Wataka Kupandishwa Madaraja.’’Kalambo’’



Na Baraka lusajo- Kalambo.
KATIKA  PICHA NI MWENYEKITI WA CWT KALAMBO
Watumishi wa umma wilayani kalambo mkoani Rukwa wamelalamikia kitendo cha wafanyakazi wa serikali walio masomoni kuto pandishwa madaraja licha ya kufuata vigezo na masharti ya utumishi wa umma wakati  wa kwenda masomoni na kuutaka uongozi wa halmashauri hiyo kutoa ufafanuzi zaidi juu ya swala hilo kwa lengo la kuondokanana sitofahamu hiyo.

KATIKA  PICHA NI  WATUMISHI  WILAYANI  KALAMBO
Wilaya ya kalambo kwa mwaka 2019/2020 imefanikiwa kupandisha madaraja watumishi wapatao 540 huku walimu wakiwa ni 455 na idara  zingine ikiwa ni 85 na huku watumishi wapatao 52 wakibadilishiwa miundo  yao ya kiutumishi.

Wakiongea kupitia kikao kazi kilichojumuisha watumishi wote wa wauma wilayani humo,wamesema  kumekwepo na changamoto ya watumishi waliomasomoni kutopandishwa madaraja licha ya kwenda  kwa  kufuata vigezo vyote.

Dosephu Ndalama mwenyekiti wa chama cha walimu wilayani humo, amesema wamekuwa  wakipata malalamiko kutoka kwa watumishi

husani walimu ambao wamekuwa wakienda masomoni bila kupandishwa madaraja.

‘’utakuta mwalimu huyu alipokuwa  anaenda masomoni  alifuata taratibu zote lakini  inakuja  kushangaza pale wengine  wanapopandishwa  madaraja lakini  wao  wamekuwa wakishindwa  kupandishwa  sasa  hili  tuanaona  sio  haki hivyo tungependa kupata ufafanuzi  zaidi kuwa kwanini walimu hawa wapati nafasi’’alisema ndalama.
Aidha aliipongeza serikali kwa  jitihada zinazofanywa na serikali ya  wilaya hiyo hususani za kupandisha  madaraja  walimu pamoja  na  watumishi  wengine wote  kwa  ujumla.

‘’tunamkupongeza  sana mkurugezi  kwa kupandisha madaraja watumnishi na mpaka  sasa kuptia ofisi ya utumishi tumeambiwa kuwa watumishi wameanza kuchukua barua zao za kupandishwa madaraja kwa hilo tunakupongeza sana.’’alisema Ndalama.

KATKA PICHA NI AFISA UTUMISHI -KALAMBO
KATIKA PICHA  NI MKURUGEZI -KALAMBO

Afisa utumishi wilayani humo Amandus Mtani amesema wamepata muongozo mpya kutoka serikalini unaolezea watumishi waliomasomoni kwa muda mrefu kuto pandindishwa madaraja.

‘’kuna muongozo mpya tumepewa  serikali ambao unaelezea watumishi waliomasomoni  kwa muda mrefu  kuto pandishwa madaraja’’alisema Mtani.
Mkurugenzi mtendaji wa hlmashauri ya Wilaya ya hiyo Msongela Mpalela, amewataka  watumishi wote kujenga mazoea ya kuchukuliana katika vituo vyao vya kazi kwa kuishi kwa amani bila migogoro kujitokeza.

‘’niwatake watumishi wangu jifunzeni kuchukulina hasa watumishi miliko huko ngazi za chin kwani mkifanya  hivyo  mtasiwisha  upendo  na amani kwenye  maeneo  yenu  ya kazi pia  lazima mkumbuke  kuwa si kila siku ni jumapili  kiongozi wako anaweza kukukasirisha kutokana na  matatizo ya  kifamilia hivyo  jifunzeni  kuchukulina’’.alisema Msongera.
KATIKA PICHA KATIBU TAWALA AKIONGEA  NA WATUMISHI


Katibu tawala  wilayani humo Frank Sichalwe amewataka  watumishi  kuacha tabia ya kuruka ngazi  hususani wakati wa kutafuta  ufumbuzi wa matatizo yao kutoka kwa viongzi husika..

Comments