Na baraka lusajo. Kalambo.
Wananchi katika kijiji cha Kalambo kata ya Mpombwe Tarafa ya Kasanga wilayani kalambo mkoani Rukwa wamejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuvamia eneo la hifadhi ya kalambo asilia na kufanya mauaji ya mnyama aina ya tembo kisha kugawana nyama kinyume na utaratibu.
Wananchi katika kijiji cha Kalambo kata ya Mpombwe Tarafa ya Kasanga wilayani kalambo mkoani Rukwa wamejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuvamia eneo la hifadhi ya kalambo asilia na kufanya mauaji ya mnyama aina ya tembo kisha kugawana nyama kinyume na utaratibu.
Akithibitha
kutokea kwa tukio hilo afisa tarafa ya Matai Endrue Manyema Ngindo amesema watu watano wanashikiliwa
na jeshi la polisi wilayani humo baada
ya kukamatwa na nyama ya tembo kufuatia msako mkali uliokuwa umefanyika kijijini hapo kufuatia kutokea kwa tukio
hilo.
katika picha ni afisa tarafa ya kasanga Endrue Ngindo |
‘’watu
watano tumewakamata wakiwa na nyara za serikali wa kwanza ni Lucas Mjanlwazira
huyu tulimkamata na nyama ya tembo,wapili ni Joseph mizyuka huyu tulimkamata
pia na nyama ya tembo,watatu ni Mejani Sipanje huyu tulimkamata na nyama ya
tembo,wa nne ni John Michael huyu pia tulimkamata na tembo na Jery Simtely huyu pia tulimkamata na mguu wa digidigi, vichwa
viwili vya ndege,Mfupa mmoja wa mamba,ganda la moja la risasi pamoja
na Ngozi ya nyoka.’’alisema Ngindo.
Aidha
Ngindo amewataka wananchi kuacha tabia ya kuvamia maeneo na hifadhi na kufanya
mauaji ya wanyama kwa lengo la kuondokana na matatizo yasiokuwa ya lazima.
Comments
Post a Comment