Wananchi Wa Kisungamile Wataka Elimu Zaidi Juu Ya Unyonyeshaji.

katika picha  ni baadhi  ya akina mama  wa kijiji  cha  kisungamile

 Na Baraka  Lusajo-Kalambo.

Wananchi katika kijiji cha Kisungamile kata ya Matai wilayani Kalambo mkoani Rukwa wameungana na watu wengine dunia kote katika kuadhimisha wiki ya unyonyeshaji ambayo ufunguzi wake ulifanyika katika eneo la Kisumba Agost moja 2019.

Kama tunavyofahamu,kuanzia tarehe  moja hadi saba Agost,kila mwaka Tanzania huungana na nchi zingine duniani kote katika  kuadhimisha wiki ya uonyeshaji maziwa ya mama. Madhimisho hayo ni fulsa ya  pekee  katika kuunganisha nguvu za wadau mbalimbali na jamii kwa ujumla ili kiufikia malengo ya azimio la Innocenti ilililofanyika nchini Italia 1,8,1990.

katika picha ni  baadhi  ya  wahudumu  wa afya
Licha ya hilo kwa ujumla lengo la madhimisho ya wiki ya unyonyeshaji yamekuwa yakilenga zaidi kumnyonyesha mtoto maziwa katika saa moja ya kwanza mara tu baada ya kujifungua sambamba na  kumyonyesha mtoto mra kwa mara.

Awali wakitoa elimu kwa wananchi wahudumu wa afya katika zahanati ya Kisungamile wamesema  uonyonyeshaji ni jukumu la kila mtu katika nafasi yake ,watu hao ni pamoja na baba ,familia ,viongozi ,ngazi ya jamii.

Baadhi ya wananchi kijijini hapo wamesema  wamenufaika  na  elimu iliotolewa  na  wahudumu  wa  afya na  kuiomba  serikali na  mashirika  binafus  kuendelea  kutoa  elimu  zaidi juu  ya  namna ya  unyonyeshaji.

Hata hivyo siku za hivi karibuni  mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo alivitaka vyombo vya  habari mkoani humo kufuatilia  na kufanya  tafiti  na kuripoti  juu matukiio mbalimbali ikiwemo haki ya akina mama kupata likizo ya uzazi  sambamba na kuandika taarifa sahihi kuhusu unyonyeshaji.

Comments