Wahasibu 80 kutoka kanda nane za TFS watoa elimu namna ya kuyatumia maporomoko ya kalambo falls.




Na Baraka  Lusajo. Rukwa.

Ziara ya mafunzo ya wahasibu themanini kutoka kanda nane za wakala wa huduma za misitu nchini-TFS- ya kuyatembelea maporomoko ya maji  ya kalambo yaliyopo wilayani kalambo mkoa wa Rukwa imetoa elimu ya jinsi ya kuyatumia maporomoko hayo kwa faida za kiuchumi wa taifa.
Katika  picha  ni mkurugezi mtendaji  wa  hlmashauri ya  kalambo  Palera  Msongela baada  ya  kutembelea  maporomoko  ya  kalambo fall na watalii kutoka nchini  swaziland.

Mhasibu mkuu wa TFS makao makuu Peter Mwakosya amesema maporomoko ya Kalambo  yanayoshika nafasi ya pili kwa urefu barani Afrika hayajatumika kikamilifu kwa ajili ya manufaa ya taifa licha ya kuwa kivutio cha kupendeza kwa watalii wa ndani na nje
Amesema wakati umefika kwa serikali kushirikiana na wadau mbalimbali katika sekta ya utalii kuboresha miundo mbinu rafiki kwa ajili ya utalii ili kusaidia kukuza pato la taifa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya jamii.

Msaidizi mkuu wa meneja wa TFS kanda ya nyanda za juu kusini Innoncent lupembe amesema hivi sasa zimefanyika taratibu za kushirikiana na mamlaka husika za utalii nchini Zambia ili kwa pamoja kuyatumia maporomoko ya kalambo kwa faida .

Josephat Chezue meneja wa wakala wa hifadhi za misutu wilayani kalambo amesema mpaka  sasa  wanaendelea  na  ujenzi  wa  nyumba za kufikia  wageni pamoja  na ngazi  za kupandia kutoka juu hadi chini na kuwataka watalii wa ndani na nje kuendelea kutembelea maeneo hayo.


ziara ya mafunzo ya wahasibu kutoka kanda zote za TFS nchini inatarajiwa kuja na ufumbuzi sahihi wa matumizi sahihi yenye faida  ya maporomoko ya Kalambo


Comments