MKUU WA MKOA WA RUKWA AWATAKA WATAALAMU WA AFYA KUTOA ELIMU YA UNYONYESHAJI WATOTO KWA WANANCHI


Na Baraka  lusajo.Rukwa-kalambo

Katika  Picha  ni mkuu  wa  mkoa Wa Rukwa  akiongea  na wanahabari ofini  kwake 
Mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo amewataka wataalamu wa afya mkoani humo kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu  ya umuhimu wa unyonyeshaji kwa akina mama wote kwa lengo la kusaidia kupata watoto wenye ulewa na afya nzuri.



Wiki ya unyonyeshaji hufanyika kuanzia tarehe moja ya kuanzia agosti moja hadi saba kila mwaka,ambapo kwa mwaka 2019 madhimisho hayo kimkoa yatafanyika katika kata ya kisusumba wilayani kalambo na huku kauli mbiu ikiwa ni ‘’mwezeshe mama aweze kunyonyesha’’

Akiongea na kituo hiki ofisini kwake mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo amesema lengo la serikali ni kuhakikisha jamii inapata uelewa kuhusu jinsi,usawa wa kijinsia,sheria na kanuni zinavyowezesha kulinda ,kuendeleza na kusaidia uonyeshaji maziwa ya mama  ili kuboresha lishe ya  watoto na jamii.

’unyonyeshaji ni jukumu la kila mtu katika nafasi yake,watu hao ni pamoja na baba,familia,viongozi ngazi ya jaamii,wafaanyakazi wa afya wenye ujuzi,wataalamu wa masuala ya uonyonyeshaji  na marafiki , pia ni vizuri kwa mama kupata muda na msaada wa kutosha katika kipindi cha kunyonyesha  na pia apate elimu ya makuzi na malezi kwa  watoto wake’’alisema Wangabo.

Alisema licha ya hilo vyombo vya habari vinaweza kufuatilia utekelezaji wa  sheria mbalimbali zinazolinda haki za uzazi na uzalishaji wa watoto kwa  kufanya tafiti ,kuandika,kuripoti matukio mbalimbali ikiwemo haki ya kupata likizo  ya uzazi.

Kaimu afisa lishe mkoani humo Asha Izina, alisema lengo la serikali ni kuhakikisha akina mama wote wanapewa  kipaumbele zaidi hususani wakati wa  kipindi cha unyonyeshaji kwa lengo la kusaidia kuondokana na adha ya  udumavu  kwa  watoto

Madhimisho ya wiki ya unyonyeshaji yatafanyika sambamba na siku ya afya ya kijiji yatakayo fanyika katika vijiji vyote kuanzia agost moja 2019 katika kijiji cha Kisumbakati  wilayani  kalambo mkoani  hapa.




Comments

  1. Asante kazi nzuri cha msingi wataramu watimize wajibu wao

    ReplyDelete

Post a Comment