Baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa limeiomba mamlaka yenye
dhamana ya ajira kumwondoa kwenye orodha ya watumishi wa halmashauri hiyo
mkaguzi wa ndani kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka.
Mwenyekiti wa baraza hilo sumuni mwanakulya amesema uamuzi huo umetolewa kwenye kikao
cha robo ya nne ya mwaka cha kujadili taarifa za utekelezaji wa shughuli
za maendeleo ya kata ishiirini na nane za halmashauri hiyo na kumtuhumu
mkaguzi Joseph Sengerema kuzuia
fedha za miradi ya maendeleo kutopelekwa kwenye vijiji na kata.
Kupiotia kikao hicho
cha baraza baadhi ya madiwani wamemtuhumu mkaguzi wa ndani wa
halmashauri hiyo Joseph Sengerema kushindwa
kumshauri vizuri mkurugenzi wa halmashauri kuhusu fedha za miradi ya maendeleo na
pia kujenga chuki kati ya wataalamu na madiwani.
kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Nkasi mhandisi Emmanuel sekwao na katibu tawala
wa wilaya hiyo cosmas kuyela wamesema
tuhuma zilizotolewa dhidi ya mkaguzi wa ndani zinafanyiwa uchunguzi kabla ya
kupelekwa kwenye mamlaka za maamuzi.
Imedaiwa katika kikao hicho cha madiwani wa halmashauri ya
wilaya ya Nkasi kuwa
viporo vya majengo ya vyumba vya madarasa na zahanati zaidi ya elfu moja mia
nne katika baadhi ya vijiji tisini vya halmashauri hiyo hayajakamilishwa
kwa kukosa fedha.
Comments
Post a Comment