Ded kalambo Akelwa Na Mila Za Wanawake Kupakwa Unga Kichwani Pindi Wanapokuwa Wamepewa Ujauzito

katika  picha ni mkurugezi mtendaji  wa  halmashauri  ya  kalambo Msongera  palela
Na Baraka  Lusajo.Kalambo

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya kalambo Mkoani Rukwa Msongera Palela amezitaka  Asasi zinazotekeleza miradi mbalimbali wilayani humo kukemea na kupinga mira potofu za wanawake kupakwa unga kichwani na kuwekewa sherehe kubwa pindi wanapokuwa wamepewa ujauzito kwa madai ya kuwa ni mashujaa.

Msongera  ameyasema  hayo wakati  wa uzinduzi wa mradi wa ukatili wa  kijinsia unaotekelezwa na Asasi ya Sucoda,ambapo amesema baadhi ya mira wilayani humo zimekuwa zikiendekezwa na wananchi  husani kwenye maeneo ya vijijini bila  kujua athari zake.

Amesema kitendo cha wanawake kupakwa unga kichjwani pindi wapatapo ujauzito ni kitendo cha kibaya kwani kinahamasisha mimba za utotoni .

‘’anapopata ujauzito anashangiliwa kuwa yeye ni shujaa, sasa mira hizi ni potofu na ukizitazama mira kama hizi utakuta zinaendekeza mimba za utotoni ‘’alisema Msongera.

Katika  picha  ni mwenyekiti wa  halmashauri yaa  kalambo akiongea na watumishi wa uma.
Amesema licha ya hilo mira hizo zimekuwa zikipelekea kujitokeza kwa vitendo vya utoro mashuleni kitu  ambacho ni hatari kwa wanafunzi kuendelea na masomo hususani wa kike.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Daudi Sichone,amesema asasi zote hazinabudi kuungana na viongozi  wa serikali za vijiji kwa kutoa mafuzo ambayo yatasaidia wao kuwaelimisha wananchi wao pindi wanakuwa  kwenye mikutano ya hadhara.

katika  picha  ni mwezeshaji  wa mafunzo   ya  ukatili  wa  kijinsiaVastina Valeli.
‘’hatuwezi kurudi nyuma kimsisingi sisi kama halmashauri ya wilaya tuna jukumu la kuwasaidia  wananchi kuondokana na chagamoto zinazowakabili.’’alisema sichone.

Vastina Valeli mwezeshaji wa mafunzo  ya ukatili  wa  kijinsia  amesema lengo ni  kuhakikisha matukio ya ukatili wa kijinsia yanatokomezwa na kusaidia kuwajengea uwezo wakuu wa idara na watumishi wengine.
katika picha  ni mkuu  wa  wilaya  ya  kalambo Julieth Binyura akiongea  na  watumishi  wa  uma.

Mkuu wa wilaya ya kalambo Julieth Binyura amewataka wananchi kushirikina na dawati la ukatili wa kinsia  katika kutoa taarifa sahihi juu ya uwepo wa matukio hayo ambayo yamekuwa yakikwamisha maendeleo  katika  jamii  zao husika.

Comments