DC. Binyura Asema Atakae Mtesa Mtoto Chamoto Kukiona.’’Kalambo’’


 Na Baraka  Lusajo.Kalambo.

Mkuu wa wilaya ya kalambo Julieth Binyura amewataka wazazi na walezi mkoani Rukwa kuwalea watoto wao katika malezi bora na kujiepusha na vitendo vya ukatili ikiwemo vipigo sambamba na kujiepusha na migogoro ya kifamilia ambayo imekuwa ikijitokeza na kusababisha tatizo la watoto wa mitaani.

katika picha  ni baadhi  ya watoto wakipatiwa  elimu  na shirika la  bethaniaa  juu  ya  umuhimu  wa haki  zao


Chimbuko la haki za mtoto lilitokana na mkataba wa kimataifa wa haki za mtoto ulioidhinishwa na Nchi  wanachama wa umoja wa mataifa mnamo novemba 20,1989 na kuridhiwa na serikali ya jamhuri ya mungano wa Tanzania Juni10,1991.

Hata hivyo kwa  kuzingatia  umuhimu wa  haki  za watoto umoja Afrika ulipitisha mkataba wa afrika wa  haki na usitawi wa mtoto mwaka 1990 na huku mkataba huo ukilenga kuhakikisha kuwa mkataba wa kimataaifa wa  haki  za mtoto unatekelezwa kwa  kuzingatia mila ,desturi,na tamaduni za kiafrika .

Kwa ujumla mikata yote  miliwili ililenga  kutoa majukumu  kwa  serikali zinazoridhia kulinda na kuendeleza haki za mtoto ili kutekeleza mikataba hiyo ambapo serikali  ya  jamhuri ya Tanzania iliandaa sera ya  maendeleo ya mtoto 2008 na kutenga, na kutunga sheria ya  mtoto Na21 ya mwaka 2009 na kanuni zake ilikuweza kutekeleza haki hizo mihimu.

katika picha ni mkuu  wa wilaya  ya kalambo


Akizindua mradi wa  kutambua  haki  za watoto uliokuwa  umeandaliwa  na shirikia la Future and Hope-(BETHANIA HOMES), mkuu  wa  wilaya  hiyo  Julieth Binyura  amesema wazazi na walezi wanatakiwa kuhakikisha watoto wao wanaendelezwa katika nyanya za kielimu,kimaadili,na kiimani.

‘‘niwasihi wazazi na walezi kuhakikisha watoto wanapewa nafasi ya kushiriki na kushirikishwa katika masuala yanayowahusu ikiwa ni pamoja kutoa maoni ,kusikilizwa na  kushiriki katika maamuzi mbalimbali katika familia na jamii kwa ujumla ‘’alisema  Binyura.

Amesema  katika  sheria ya  mwaka  2009 mtoto  anahaki  mbalimbali  katika  jamii ikiwemo kupata  haki  ya  kuishi,kupumzika kuheshimiwa na kuthaminiwa.
katika picha  ni mratibu  wa Shirika la  Bethania akitoa elimu  kwa  wananchi

Joseph Kasaila mratibu wa tasisi ya Future and Hope –BETHANIA HOMES,amesema wamelazimika  kupeleka mradi huo utahudumu katika eneo la Matai wilayani kalambo na kusema lengo kubwa ni  kuhakikisha wananchi wanapata ulewa juu ya umuhimu wa kuwalea watoto kwa lengo la kupunguza wimbi la watoto wa mitaani.

‘’mfano watoto  wanao pitia adha  hiyo  ni wanaopitia hali hii  ni  wale ambao waliofiwa na wazazi wote wawili(yatima) watoto wanaohusishwa na huduma za kingono  kinyume na  sheria ,watoto wanaofanya kazi mogodini ,watoto wanaokinzana na sheria ,watoto wanaoishi na  kufanya kazi mitaani ,watoto wenye ulemavu na  watoto wenye mambukizi  ya VVU na UKIMWI.’’alisema Kasaila
katika picha  ni kaimu mkurugezi akitoa  elimu  kwa wananchi

Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo yasita Nkyabonaki,amesema kila mzazi anatakiwa kuhakikisha  waatoto  wanalelewa  katika  misingi  bora  na tabia  njema.
 ‘’marekebisho yanaanziakatika ngazi ya familia na jamii ,ambapo wazazi /walezi na wanajamii wanajukumu kubwa la kuhakikisha kuwa kila mtoto analelea na kukua kwa  kufuata maadili,mila ma destruri za jamii husika.’’alisema Nkyabonaki.


Comments