Das Kalambo Awagiza Watumishi Wa Umma Kusajili Simu Kwa Njia Ya Mtandao

Katika  picha  ni katibu  tawala  wilayani  kalambo



Uongozi wa serikali wilayani Kalambo mkoa wa Rukwa umewaagiza watumishi wote wa umma wilayani humo kusajili laini za  simu zao za mitandao mbalimbali kwa njia ya alama za vidole ili kuimarisha utendaji wao bora wa kazi.

Akizindua zoezi la mkakati wa kusajili laini za simu wilayani kalambo katibu tawala  wilayani wilayani humo Frank Sichalwe, amesema usajili huo utawawezesha watumishi hao kutoa huduma inayostahili kwa wakati unaostahili na kusaidia kuchochea shughuli za  maendeleo ya jamii.

Amesema zoezi hilo litatawahusu watu wote kutoka maeneo ya vijijini na mijini na kusema   kwa sasa  wameanza na watumishi  wote  wilayani humo kwa kupatia elimu.

Baadhi ya wakazi wa mji mdogo wa matai wilayani kalambo mkoa wa Rukwa wameelezea umuhimu wa kusajili laini za simu kwa njia ya alama za vidole na kusema utaratibu huo utalinda usalama wa mteja kutokea  uwezekano wa kufanyiwa vitendo vya uhalifu na watu wenye nia ovu.
Mkuu wa mamlaka ya mawasiliano-tcra- kanda ya nyanda za juu kusini mhandisi  Asajile  John, amesema lengo la serikali katika kutekeleza zoezi hili ni kutoa wigo mpana wa kuthibiti uhalifu wa mtandaoni na kuthibiti matumizi mabaya ya simu ambapo kawia ntemo afisa usajili kutoka mamlaka ya vitambulisho vya taifa-nida-anaelezea changamoto zilizopo.
mamlaka ya mawasiliano-tcra- kanda ya nyanda za juu kusini inaendesha zoezi la kuhamasisha usajili wa laini za simu kwa njia ya alama za vidole katika mikoa ya Rukwa na Katavi kabla ya ukomo wa zoezi hili mwezi december mwaka huu


Comments