TAARIFA ZA HIVI PUNDE. Club Ya Simba Wiayani Nkasi Yatoa Misaada Kwa Watoto Yatima.


Na Israel Mwaisaka,Nkasi

Baadhi  ya  mashabiki wa simba  wakitoa  misaada watoto yatima.
Wanachama wa club ya simba wilayani Nkasi mkoani Rukwa wametoa msaada kwenye kituo cha watoto yatima cha kilangala mission kama njia ya kusherehekea wiki la simba day.
 Akikabidhi msaada huo kwaniaba ya wanachama hao wa simba donal mkama alisema kuwa msaada huo walioutoa wa vitu mbalimbali una thamani ya zaidi ya tshs,500,000 na fedha hizo zimetokana na michango mbalimbali kutoka kwa wanachama.
alisema kuwa wao kama tawi la simba wilayani Nkasi walikaa na kutafakari nini cha kufanya katika wiki hili la simba day na wakaonelea kuwa kuna umuhimu wao kwenda kuungana na watoto yatima katika kituo cha kilangala ambao wanapata tabu sana kutokana na mazingira nagumu waliyonayo.
alifafanua kuwa wanachama wote kwa ujumla walikubaliana kuwa wao kama marafiki wa simba wanalojukumu la kufanya siku hiyo kwa jamii na kila mmoja aliguswa na ambavyo watoto yatima wanavyokabiliwa na changamoto mbalimbali na kuamua kuchanga fedha ili kutoa msaada kwa kituo hicho.
Albert Nayingo mmoja wa wanachama hao amedai kuwa wao kama wanachama wa simba wataendelea kufanya  shughuli mbalimbali za kijamii hata kama wiki la simba day litakwisha kwani club yao imelenga kuwasaidia jamii kutokana na changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo.
kwa upande wake Francis Mkemwa alidai kuwa kwa sasa club yao ina wanachama wengi na hivyo wanao mfuko mkubwa na kuwa fedha walizozitoa ni sehemu tu ya zile zilizopo kwenye mfuko wao na kuwa lengo lao sasa ni kuendelea kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii ili kuweza kuisaidia jamii yenye shida.
Akipokea msaada huo msimamizi msaidizi wa kituo cha watoto yatima kilangala Mission Velonica wakalanda aliishukuru club ya simba tawi la nkasi kwa uamuzi huo wa kuwapelekea msaada huo na kuwa kwa kipindi hiki walikua na 

Comments