CCM Ya ipongeza Ofisi Ya Mkuu Wa Wilaya Ya Kalambo Kwa Kutoa Misaada


Na baraka  lusajo. Kalambo.
katika picha ni mwenyekitri  wa ccm wilaya  ya kalambo.

Chama cha mapindizi CCM wilayani Kalambo mkoani Rukwa kimeipongeza ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo kwa kutoa vifaa mbalimbali vya ujenzi kwa ajili ya umaliziaji wa maboma pamoja na ukarabati wa majengo ya shule na zahanati .

Ofisi ya mkuu wa wilaya ya kalambo imekuwa na utaratibu wa kutoa misaada kila mwaka kulingana na uhitaji wa maeneo husika,ambapo kwa mwaka huu iilitoa vifaa vya ujezi ikiwemo bati na saruji na  kuwakabithi watendaji na madiwani kwa lengo la kusaidia umaliziaji wa majengo kwenye kata na vijiji  tofauti vilivyopo wilayani humo.

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM wilayani humo Alfred Mwanga amesema  kwa ujumla ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo nimekuwa ikijitahidi kwa kiwango kikubwa kutatua changamoto za wananchi  hususani maeneo ya vijijini.
‘’tunakupongeza kutoa misaada hii,lakini madiwani wapo, watendaji wapo,wenyeviti wa vijiji wapo  hivyo sitegemei kuona eti sikumoja unapewa  taarifa kuwa misaada ulitoa haikutumika vile inavyotakiwa na wakati wahusika wote wapo itakuwa ni majabu ‘’alisema Mwanga.

Mbali na hayo amelaani vikali kitendo cha baadhi ya viongozi kuto unga mkono jitihada zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya mungano waTanzania John Paombe Maghufuli  nakusema watu hao si  wema katika taifa hili.
katika picha ni mkuu  wa wilaya  ya kalambo akitoa misaada

Mkuu wa wilaya hiyo Julieth Binyura amewataka wananchi pamoja na  wachungaji  kuendelea kumuombea Rais Wa Jamhuri ya mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa  anayo ifanya .

Hata hivyo kwa mwaka 2019 ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo imetoa  misada ya vifaa vya ujezi kwa mashirika ya dini,watu binafus pamoja na kwenye taasisi ya za serikali vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni tano.



Comments