Ajali Ya Morogoro Ya Kwamisha Ziara Ya Kangi Lugola Mkoani Rukwa

katika picha  ni waziri  wa  mambo  ya ndani  kangi  lugora.


Na Baraka  lusajo .Rukwa.

WAZIRI wa Mambo ya ndani ya Nchi Kangi Lugola ameahirisha ziara yake mkoani Rukwa iliyokua imeanza leo kutokana na ajali iliyotoke leo alfajiri mkoani Morogoro .

Akizungumza na Waandishi wa habari mjini  Sumbawanga amesema kuwa amepata taarifa kutoka kwa kamishina jenerali wa jeshi la zima moto Thobias Andengenye juu ya ajali  iliyotokea mjini Morogoro katika maeneo ya Msamvu ikihusisha gari la mafuta na kuua watu kadhaa .

Alisema kuwa ajari hiyo iliyotokea imehusisha Watu wengi na ambao idadi yake bado hajaipata sawasawa na kuwa kutokana na mazingira hayo ameamua  kuiahirisha ziara hiyo mkoani Rukwa ili aweze kwenda kuungana na watanzania wengine juu ya msiba huo mkubwa.

Alidai kuwa bado kuna tatizo kubwa la matumizi ya barabara kwa watu wote na kuwa kama sheria ya Usalama barabarani  Sura 168 itatumika sawasawa kwa watumiaji wa barabara  kuna uwezekano mkubwa wa ajali kama hizo zikaweza kuepukwa.


Lugola alifafanua kuwa licha ya sheria hiyo ya usalama barabarani kuwepo serikali ipo kwenye mchakato wa kuitunga sheria mpya ya Usalama barabarani na kuwa sheria hiyo mpya ipo mbioni na itaanza kufanya kazi ili kuweza kukabiliana na ajali zisizokuwa za lazima na kuweza kupoteza maisha ya watu wasiokua na hatia.

Alidai kuwa jeshi la Polisi mkoani Morogoro limefanya kazi  kubwa ya kuwatawanya watu waliokuwa katika eneo la tukio vinginevyo hari ingekua mbaya zaidi na kutoa wito kwa jamii kutokimbilia katika maeneo yanapotokea majanga hususani ya moto kama ilivyokuwa mkoani morogoro .
katika  picha ni  mkuu wa  mkoa  wa  Rukwa  Joachim Wangabo.

Hata hivyo mkuu wa mkoa  wa  Rukwa  Joachim Wangabo  ametuma  salamu  za rambirambi   kwa  mkuu wa mkoa  wa  morogoro  kufuatia  kujitoza  kwa  ajali  hiyo.





Comments