Na Baraka Lusajo - Rukwa
Jeshi la polisi mkoani Rukwa limeripoti matukio mawili tofauti likiwemo la watu 5 kukamatwa na risasi 1493 za silaha za kivita aina ya AK 47 na SR huku watu wawili kati ya hao wakikamatwa na risasi 14 za Shotgun pamoja na vipande 31 vya gamba la kobe kinyume na sheria.Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Rukwa ACP William Mwampagale alisema baada ya kupata taarifa fiche kwa kushirikiana na raia wema walifanikiwa kuwakamata watu watatu wakiwa na risasi 1493 za silaha za kivita aina ya Ak 47 na SAR kinyume cha sheria.
Alisema
katika uchunguzi wa awali walibaini kuwa wavuvi 7 walizikuta risasi hizo zikiwa
mapangoni wakidhani ni madini ya dhahabu.
‘’Watuhumiwa
hao walikamatwa na walipohojiwa walishindwa kuelezea walikuwa wanazipeleka wapi
ingawaje walizitambua kuwa ni risasi za moto. upelelezi wa kina Zaidi unaendelea
ili kubaini nia yao’’ alisema kamanda Mwampagale
Aidha katika tukio la pili jeshi hilo linawashikilia watu wawili baada ya kuwakamata katika eneo la Kashai Edeni ‘’B’’ kata ya Momoka manispaa ya sumbawanga mkoani Rukwa na kwamba walipatikana wakiwa na risasi 14 za shotgun.
‘’Pia
watu hao walipatikana wakiwa na vipande 31 vya gamba la kobe pamoja na nyamapori
vipande viwili, manyoya nungunungu vipande 2 na
mishale 2 ambayo huwawezesha katika kutekeleza vitendo vya ujangili.Watuhumiwa hawa
watafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika.
Comments
Post a Comment